Maombi yenye Mafanikio ni kitabu kinacholenga kuimarisha uhusiano baina ya Mungu na mwanadamu kupitia maombi. Kitabu
hiki kitakusaidia kutambua mambo makuu matano; Mungu unayepaswa kumwomba, mambo unayotakiwa kuomba, mahali
panapofaa kwa ajili ya maombi, wakati wa kufanya maombi na namna ya kumwomba Mungu.
Kitabu hiki kina sura kuu tisa ambazo ni; ukweli kuhusu maombi, aina na kukua katika maombi, wakati unaofaa kumwomba
Mungu, namna ya kuandaa maombi, jinsi ya kuomba, mambo yanayozuia maombi, majibu ya maombi, kufunga na kuomba, na
maombi na kanisa la leo.
Kupitia kitabu hiki utatambua kuwa unapaswa kumwomba Mungu siku zote pasipo kukata tamaa na sio kumwomba Mungu
wakati wa mahitaji au matatizo tu.
Luka 18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.”